Sunday, 26 June 2016

VIDEO:Waziri mkuu wa Uingereza ajiuzulu baada ya kura za maoni kuonesha raia wa taifa hilo kutaka kujitoa kwenye umoja wa ulaya.

cameroon on press 001

Akionekana mwenye huzuni,Waziri mkuu wa Uingereza Davidi Cameron amesema kuwa atasalia ofisini kwa siku tisini zijazo  kabla ya kung’atuka rasmi kwenye wadhifa huo.
Bw Cameron ambaye ameongoza kampeini ya Uingereza kusalia katika muungano wa umoja wa ulaya  (EU) amesema uamuzi wa raia wa taifa hilo kubwa dunaini kujitoa kwenye umoja wa ulaya  umempa mshutuko mkubwa ikiwa ni pamoja na  watu mashuhuri duniani.
cameroon with his wife 0003                     David Cameron na mkewe Samantha.
Akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari nje ya afisi yake jijini London, Bwana Cameron amedai kuwa anahisi yeye sio mtu muhimu wa kuliongoza taifa hilo kwa ufanisi chini ya uamuzi kama uliofikiwa na raia wanaopendekeza Uingereza kujitoa kwenye umoja wa ulaya.
ungereza poll result
Kwa upande wa waliokua wakiongoza kampeni kwa taifa hilo kujitoa,wameonekana kusheherekea matokeo hayo.
leave camp 001
leave camp 002
leave camp 004
leave camp 003
leave camp 005
leave camp 006Kiongozi mkuu wa muungano wa Ulaya Donald Tusk amesema kuwa mataifa y 27 yaliyosaliwa kwenye umoja huo (EU) yataendelea na ushirikiano na kuongeza kuwa mataifa 6 wanachama wakuu wa muungano huo wa Ulaya yatakutana jumamosi hii kujadili hatma ya muungano huo ambao bado sasa unatishiwa na kujiondoa kwa mataifa mengine ambayo pia yanakabiliwa na shinikizo la kujiondoa.

No comments:

Post a Comment