Carroll, 27, alikuwa amewafungia West Ham mabao mawili katika mechi zake nne za majuzi zaidi baada ya kurudi kucheza Septemba 2015.
Kabla ya hapo, alikuwa amekaa miezi saba nje baada ya kufanyiwa upasuaji kwenye goti lake.
“Mambo yakienda tunavyotarajia, basi atatusaidia mechi 10-15 za mwisho msimu huu,” amesema meneja wa West Ham Slaven Bilic.
West Ham wamo nambari tano ligini, alama moja pekee nyuma ya Tottenham walio nambari nne, zikiwa zimesalia mechi 17 za kuchezwa msimu huu.
No comments:
Post a Comment