Basi la Manchester
United lilishambuliwa kwa mawe lilipokuwa linaelekea katika uwanja wa
Upton Park ambao unamilikiwa na wapinzani wao katika mechi ya jumanne
jioni West Ham.
Shambulizi hilo lilisababisha mechi baina ya Manchester United na West ham kucheleweshwa kwa zaidi ya dakika 45.
Basi hilo lilishambuliwa kwa chupa na mawe.
''ilikuwa tukio la kushtua sana , haikufurahisha kabisa kushambuliwa na mashabiki wa timu pinzani hadi gari letu linaharibiwa'' alisema nahodha wa Manchester United Wayne Rooney
Ninaamini West Ham hawatafurahia kuona walichofanya mashabiki wao.
Timu hiyo inatarajiwa kuhamia makao yao mapya ya Olympic Stadium.
Aidha uwanja huo wa Upton unafahamika pia kama Boleyn Ground.
Kocha wa Manchester United Louis van Gaal alinukuliwa akisema kuwa hana cha kusema ila angependa picha zenyewe zijieleze.
No comments:
Post a Comment