Mama mmoja raia wa Australia ametoa picha za mapacha watano aliowazaa mwezi Januari.Kim Tucci wa miaka 26 alichukua dadika mbili tu kujifungua wanawe hao, wasichana wanne na mvulana mmoja.
Wote walitungwa kawaida, hakutumia matibabu yeyote ya uzazi. Madaktari 50 walimsaidia mama huyo kujifungua kwa
njiya ya upasuaji, na wanawe wote wako shwari.Wanasayansi wanasema ni
mama mmoja kati ya milioni 55 ana nafasi ya kuzaa mapacha watano.
Bi
Tucci alipata umaarufu sana wakati alipoweka taarifa za mimba yake
katika ukurasa wake wa Facebook.Kampuni ya kunasa picha ya Erin
Elizabeth imesaidia sana kunadi safari ya Bi Tucci wakati wa uja uzito
wake. Mama huyo ameelezea changamoto alizokumbana nazo
akisema kwa wakati mmoja alihisi kama anapoteza maisha.Ameongeza
madaktari walimshauri kuwaokoa watoto wawili na kumtaka kuwatoa wengine
kutokana na sababu za kiafya.
Hata hivyo aliamua kubeba mimba yake hadi mwisho.
Bi
Tucci na mumewe bwana Vaughn wana watoto watatu mvulana na wasichana
wawili.Wameanza kuchangisha pesa ili kununua gari kubwa ambalo litaweza
kukimu familia hiyo kubwa.
No comments:
Post a Comment