Wednesday, 13 July 2016

Venance Mwamoto ataka madawati yenye viwango


Image result for venance mwamoto
Venance  Mwamoto


MBUNGE  wa   jimbo la  Kilolo  mkoani Iringa Venance  Mwamoto  amewataka   walimu  wakuu wa  shule  na kamati  za  shule  wilayani   humo   kuhakikisha   wanapokea  madawati yenye  kiwango kinachotakiwa.
Mwamoto  ameyasema  hayo     wakati  akizungumza na  wananchi  wa  kijiji  cha Idegenda  wakati  na kuongeza kuwa mfuko wa Jimbo ulitoa shilingi milioni 30   kwa  ajili ya  kutengeneza madawati  600   ili  kumaliza  tatizo  la  uhaba wa madawati  katika  wilaya   ya  Kilolo.

Amesema  lengo la  kutoa  pesa  hizo  ni kuona  madawati  yanayotengenezwa  yanakuwa na  kiwango kizuri ili  wanafunzi   waweze   kuyatumia  kwa  muda  mrefu  na  sio  kuendelea   kutengeneza madawati  kila mwaka.

Amesema pesa hizo ni za wananchi wa Kilolo hivyo hajakubaiana na  kiwango  cha  ubora  wa madawati  hayo na kulazimika  kuyakataa madawati hayo  na  tayari  mkuu  wa  mkoa  wa  Iringa Bi.Amina Masenza naye ameyakataa madawati hayo 745 na mengine ambayo  idadi yake inafika zaidi ya madawati  10000

Nao  uongozi wa  shule  ya  Msingi Idegenda  umemweleza  mbunge  huyo  katika  mkutano  huo   kuwa  madawati zaidi ya 200  ambayo shule    hiyo  imepokea  hayana  ubora na  hivyo  walichokifanya ili  kuepuka  kuwajibika  kwa  kushindwa  kusimamia  madawati  hayo   wamelazimika  kuchagua madawati  yote mabovu na  kuyahifadhi stoo  .

No comments:

Post a Comment