Monday, 28 December 2015

DIWANI NYARUSI : MADIWANI FANYENI KAZI KURUDISHA FADHIRA KWA WANANCHI



Image result for frenk nyarusi diwani kata ya mivinjeni Madiwani pamoja na viongozi wa serikali za mitaa wameshauriwa kurudisha fadhira kwa wananchi kwa kufanya kazi kwa bidii na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Hayo yamesemwa hii leo katika ofisi za CHADEMA wilaya ya Iringa na na mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo wilaya ya iringa Frenk Nyarusi ambaye pia ni diwani wa kata ya mivinjeni na kuongeza kuwa madiwani pamoja na viongozi wa serikali za mitaa jukumu lao kubwa ni kuwatumikia wananchi hata bila kuhitaji fedha kutoka kwao.

Aidha nyarusi amebainisha kuwa kuna baadhi ya viongozi ambao siyo waadilifu wamekuwa wakijihusisha na kuomba fedha wanapotoa huduma kwa wananchi pia amesema kuwa hawatasita kuchukua hatua kwa wale viongozi ambao watabainika na tuhuma hizo.

Hata hivyo nyarusi amewataka madiwani kuzikumbuka ahadi walizo ahidi na kuzitekereka kwani kutofanya hivyo watakuwa wanajiwekea mazingira magumu wao wenyewe kwenye chaguzi zijazo.

No comments:

Post a Comment