Sunday 3 July 2016

Hizi ndizo sababu za Boss wa label ya mavazi na vifaa vya michezo ya ‘NIKE’ kujiuzulu.


Mwanzilishi wa label ya mavazi,mitindo na vifaa vya michezo ya ‘NIKE’,Phil Knight ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake kama mwenyekiti wa wa bodi ya label hiyo kubwa ya mavazi duniani huku umri wake ukitajwa kama sababu ya kujiuzulu kwake.
Phil Knight ambae utajiri wake unakadiriwa kufikia kiasi cha dola $25 bilioni amepanga kuugawa sehemu ya fedha zake kwenye mashirika ya kusaidia watu wenye mahitaji maaulumu kama wagojwa,yatima na wakimbizi.
Nafasi inatarajiwa kuchukuliwa na Mark Parker ambapo Mkurugenzi mkuu wa wa kampuni ya Apple’s Tim Cook akitajwa kuwa afisa mipango wa kampuni hiyo katika kipindi cha mpito.
“Phil’s impact on Nike is immeasurable,” …… “His entrepreneurial drive is and always will be part of our DNA. Along with Nike’s exceptional management team, I am committed to leading our next era of innovation and growth as we serve and inspire athletes throughout the world”.Alisema Mark Parker,Mkurugenzi mpya wa ‘NIKE’.
Phil Knight mwenye umri wa miaka 78,anadaiwa kuuza hisa zake kwenye label ya mavazi inayofahamika kama ‘Swoosh LLC’,ambayo ni sehemu ya wabia wa NIKE,ambapo hisa hizo zitamilikiwa na mwanae wa kiume anaefahamika kama Travis huku akimiliki kura mbili kati tano kwenye maamuzi ya bodi,wakati kura tatu zilizosalia zikimilikiwa na Parker,Alan Graf Jr na John Donahoe.

No comments:

Post a Comment