![]() |
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Lameck Nchemba akila kiapo mbele ya rais Magufuli |
Rais wa Tanzania
Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha mawaziri wapya wa mambo ya ndani
na yule wa kilimo siku mbili tu baada ya kutangaza mabadiliko madogo
katika baraza lake la mawaziri.
Jumamosi iliyopita rais Magufuli
alitangaza uteuzi wa mbunge wa Buchosha Dkt. Charles John Tizeba kuwa
waziri wa kilimo, mifugo na uvuvi.Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Waziri wa Kilimo, bwana Mwigulu Lameck Nchemba aliteuliwa kuwa Waziri wa mambo ya ndani ya nchi.
![]() |
Rais Magufuli ampongeza waziri Nchemba kwa wadhifa wake mpya |
Mawaziri hao walikula kiapo cha uaminifu kwa rais na jamhuri ya tanzania saa tatu asubuhi katika ikulu ya rais jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment