Rais Kenyatta alisema Kenya inathamini sana urafiki wa karibu ambao umekuwepo na kwamba anatarajia urafiki huo pamoja na ushirikiano hasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki utaendelea.
“Namtakia Rais Museveni ufanisi anapoendelea kutumikia taifa lake kwa muhula mwingine. Yeye na Uganda wanaweza kutarajia uungaji mkono wangu, na urafiki kutoka kwangu, pamoja na kutoka kwa kaka na dada zao hapa Kenya.”
Lakini hatua hiyo haikuwafurahisha baadhi ya Wakenya mtandaoni na wengi waliandika wakimshutumu.
Saa chache baadaye, kitambulisha mada#UhuruIsNotKenyakikaanza kuvuma kwenye Twitter. Kwenye Facebook, wengi waliandika kumkosoa.
Wengine walishangaa ni kwa nini Rais Kenyatta akaharakisha kumpongeza Rais Museveni ilihali “alichukua muda kumpongeza Dkt John Magufuli” alipotangazwa mshindi Tanzania”.
Kesi dhidi ya Rais Kenyatta iliondolewa lakini kesi dhidi ya Naibu Rais William Ruto na mwanahabari Joshua arap Sang inaendelea.
Rais Museveni amehudhuria sherehe kadha za kitaifa na kupewa muda wa kuwahutubia wananchi
No comments:
Post a Comment