EMIRATES FA CUP
Ratiba/Matokeo:
Raundi ya 5
Jumamosi Februari 20
Arsenal 0 Hull City 0
Reading 3 West Brom 1
Watford 1 Leeds United 0
2015 Bournemouth v Everton
Mabingwa Watetezi wa FA CUP Arsenal itabidi waende huko KC Stadium kurudiana na Hull City baada ya Leo kutoka Sare 0-0 Uwanjani Emirates katika Mechi ya Raundi ya 5 ya EMIRATES Fa cup.
Kila Timu ilifanyika mabadiliko makubwa katika Vikosi vyao vilivyocheza Mechi zao zilizopita kwa Arsenal kubadili Wachezaji 9 na Hull City 10 lakini Arsenal wakashindwa kuipenya ngome ya Hull huku Kipa wa Vinara hao wa Daraja la chini la Championship wakijilinda imara kwa Kipa wao, Eldin Jakupovic, kuokoa Bao kadhaa za wazi.
Katika Mechi nyingine za Raundi ya 5 ya FA CUP zilizochezwa Leo Readuing, inayocheza Championship, iliitwanga West Brom ya Ligi Kuu England Bao 3-1 baada ya kutoka nyuma kwa Bao la Dakika ya 54 la Darren Fletcher nas kubamiza 3 zao kupitia Paul McShane, Dakika ya 59, Michael Hector, 72, na Lucas Piazon, 94.
Nao Watford wameitungua Leeds United 1-0 kwa Bao la kujifunga mwenyewe Scott Wootton la Dakika ya 53.
VIKOSI:
Arsenal: Ospina; Chambers, Mertesacker, Koscielny, Gibbs; Flamini, Elneny, Campbell, Iwobi, Welbeck, Walcott.
Akiba: Macey, Bellerin, Monreal, Coquelin, Oxlade-Chamberlain, Alexis, Giroud.
Hull City: Jakupovic; Taylor, Davies, Maguire, Tymon; Bruce, Meyler; Elmohamady, Powell, Maloney; Diomande.
Akiba: Kuciak, Huddlestone, Hernandez, Diame, Aluko, Robertson, Odubajo
REFA: Mike Dean
EMIRATES FA CUP
Raundi ya 5
Jumapili Februari 21
1700 Blackburn v West Ham
1800 Tottenham v Crystal Palace
1900 Chelsea v Man City
Jumatatu Februari 22
2245 Shrewsbury v Man United
THE EMIRATES FA CUP 2015/16
TAREHE MUHIMU
Raundi ya 3
Ijumaa 9 Januari 2016
Raundi ya 4
Jumamosi 30 Januari 2016
Raundi ya 5
Jumamosi 20 Februari 2016
Raundi ya 6-Robo Fainali
Jumamosi 12 Machi 2016
Nusu Fainali
Jumamosi 23 Aprili 2016 & Jumapili 24 Aprili 2016
Fainali
Jumamosi 21 Mei 2016
No comments:
Post a Comment