Zephany Nurse aliibiwa kutoka kwa kitanda cha mamake siku ya pili tu baada ya kuzaliwa.
Inadaiwa mwanamke huyo alimlea kijana huyo kama mwanaye.
Mtuhumiwa anasemekana kumfanya mamake msichana huyo rafikiye wa karibu alipokuwa bado hospitalini kabla ya kumuiba.
Alimsihi mamake kumsaidia mtoto ili aweze kulala.
Baadaye mfanyikazi wa hospitali hiyo alimuamusha na kumuarifu kuwa mtoto wake ametoweka.
Alipatikana miaka 18 baadaye, baada ya dadake kuwaambia wazazi wake kuna mwanafunzi shuleni mwake wanayefanana naye kama shilingi kwa ya pili.
Uchunguzi wa kina wa vinasaba ulidhihirisha wasichana hao ni ndugu wa baba mmoja na mama mmoja.
No comments:
Post a Comment