Wednesday, 2 December 2015

Barcelona waendelea kutoa dozi kama kawaida kwa Villanovense baada ya kutoa dozi kama hiyo kwa Roma (+Pichaz&Video) copa del rey

Usiku wa December 2 ilikuwa ni zamu ya kuchezwa kwa mechi za Copa del Rey nchini Hispania, michezo nane ilichezwa usiku wa December 2 ila mchezo uliyochezwa mapema zaidi ni mchezo kati ya FC Barcelona dhidi ya Villanovense uliyopigwa katika dimmba la Nou Cam
2EFFB0E400000578-0-image-a-8_1449088000749
Kwa sasa FC Barcelona unaweza kuita ndio timu inayoongoza kwa safu bora ya ushambuliaji kutokana na ushindi wa mechi zao za hivi karibuni kuibuka na ushindi wa idadi kubwa ya magoli, matokeo ya mechi zao nne zilizopita zinaonesha kuwa walimfunga Real Madrid 4-0 LALIGA, wakamfunga AS Roma 6-1 UEFA, wakamfunga Real Sociedad 4-0 na usiku wa December 2 wameifunga Villanovense goli 6-1 katika mchezo wa Copa del Rey.
2EFFEFA700000578-0-Less_than_two_minutes_later_and_young_forward_Sandro_Ramirez_dou-a-11_1449088218362
Kwa takwimu hizo FC Barcelona wanakuwa wamefunga jumla ya 20 ndani ya mechi nne ambapo ni wastani wa goli 5 kwa kila mechi, magoli ya FC Barcelona yamefungwa na Daniel Alves dakika ya 4, Sandro Ramirez dakika ya 21, 31, 69 na  Munir El Haddadi dakika ya 51 na 76 wakati goli pekee la Villanovense lilifungwa na Juanfran dakika ya 29.







No comments:

Post a Comment