Wednesday, 2 December 2015

Watu ishirini wapigwa risasi Marekani

Image result for SIGN OF BREAKING NEWS Takriban watu 20 wameshambuliwa na takriban mtu mmoja kwa risasi mjini San Bernadino mashariki mwa Los Angeles.
Idara ya Polisi mjini humo imesema tukio hilo inawezekana lilihusisha watu wenye silaha mpaka watatu tukio lililotokea kwenye kituo cha huduma kwa watu wenye ulemavu.
Msemaji ameeleza kuwa mashuhuda waliwaona watu wakiwa na silaha walioaminika kuvalia mavazi ya kukinga risasi.
Picha za Televisheni zimeonyesha watu wakiondolewa kutoka kwenye jengo.
Taarifa zaidi tutawaletea kwa kadri tutakavyokuwa tunazipata.


KWA HABARI ZAIDI ENDELEA KUTUFUATILIA NDANI YA HABARIKA TZ TUTAKUSOGEZEA KILA KITU...........

No comments:

Post a Comment