Mabingwa wa La Liga Barcelona Jana wameitandika Eibar Bao 3-1 huko Nou Camp kwa Bao za Luis Suarez.
Eibar ndio walitangulia kufunga kwa Bao la Bojan Baston na Barca kujibu kwa Bao 3 za Luis Suarez za Dakika za 21, 48 na 85.
Katika Dakika ya 83 Mchezaji wa Barca Javier Mascherano alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Ushindi huo umewanyanyua Barca hadi Nafasi ya Pili wakilingana kwa Pointi na Vinara Real Madrid ambao wana ubora wa Magoli.

No comments:
Post a Comment