Monday, 26 October 2015

JOSE MOURINHO MAJI YA MFIKA SHINGONI SASA



 Image result for MORIHNO



Zipo ripoti zimezagaa huko England kuwa Meneja wa Chelsea Jose Mourinho atafukuzwa kazi ikiwa Timu yake itafungwa na Liverpool kwenye Ligi Kuu England.

Ripoti hizo zimedai Mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich, ameghadhibika baada kuiona Timu yake ikichapwa 2-1 huko Upton Park na West Ham hapo Jumamosi Siku ambayo ilikuwa ni Sherehe ya Bethdei yake.
 
Kipigo hicho cha Mechi hiyo kimewatupa Chelsea, ambao ni Mabingwa Watetezi, Nafasi ya 15 kwenye Ligi Kuu England wakiwa Pointi 11 nyuma ya Vinara Man City baada ya Mechi 10 kuchezwa.
Juu ya kipigo hicho, kwenye Mechi hiyo, Mourinho, Msaidizi wake Silvino Loura na Mchezaji wake Nemanja Matic wote walitolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
 
Jumanne Chelsea, ambao pia ni Mabingwa Watetezi wa Capital One Cup, wapo Ugenini kuchezi Mechi ya Raundi ya 4 ya Kombe hilo na Timu isiyotabirika Stoke City.
 
Lakini Mechi inayodaiwa ndio itamfukuzisha kazi Mourinho ni ile ya Ligi ya Jumamosi dhidi ya Liverpool ambayo sasa iko chini ya Mjerumani Jurgen Klopp.
 
Klopp, alipokuwa Borussia Dortmund Mwaka 2013, aliwahi kuitwanga Real Madrid chini ya Mourinho Bao 4-3 kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI.
 
 

No comments:

Post a Comment