Mradi wa kuunda
gari liendalo kasi Zaidi duniani umefufuliwa na gari hilo linatarajiwa
kujaribu kuvunja rekodi ya dunia mwaka ujao.
Mpango wa kuunda gari hilo lililopewa jina Bloodhound ulikwama miezi ya karibuni kutokana na matatizo ya kifedha.Oktoba 2017 itakuwa miaka 20 tangu kuwekwa kwa rekodi ya sasa ya kasi ya gari ardhini ambayo ni kilomita 1,228 kwa saa (763mph).
Rekodi hiyo iliwekwa na gari lililopewa jina Thrust SSC jangwani Marekani.
Gari hilo linaundiwa Uingereza.
Gari hilo liliwasilishwa kwa maonesho Canary Wharf, London likiwa bado halijakamilika mwezi Septemba mwaka jana.
Tangu wakati huo, limekuwa Bristol likiwa halifanyiwi kazi yoyote.
Gari hilo litatumia injini ya ndege aina ya Eurofighter-Typhoon ambayo itaundwa na kampuni ya Nammo ya Norway.
Gia yake itaundwa na wahandisi wa mradi huo wa Bloodhound na pampu yake itakuwa ya Jaguar V8.
Litafanyiwa majaribio Cornwall, Uingereza mwezi Mei au Juni mwaka ujao.
No comments:
Post a Comment