Friday, 15 January 2016

TUZO YA UBORA LIGI KUU ENGLAND-DESEMBA: WATFORD WAZOA KWA MENEJA NA MCHEZAJI BORA!

Watford
MENEJA wa Watford, Quique Sánchez Flores na Mchezaji wake, Odion Ighalo, ndio wametunukiwa Tuzo za Meneja Bora na Mchezaji Bora za Ligi Kuu England kwa Mwezi Desemba zinazotolewa na Wadhamini wa Ligi hiyo, Barclays.
Kikosi cha Flores kilizoa Pointi 10 katika Mechi zao 5 za Mwezi Novemba kwa kuzifunga Norwich, Sunderland na Liverpool na kutoka Sare na Chelsea na kupanda kuwa kwenye Timu 10 za juu kwenye Msimamo wa Ligi.
Flores, anaetoka Spain, amewabwaga Arsène Wenger, Claudio Ranieri na Alan Pardew kwa kutwaa Tuzo hii.
Nae Ighalo, Mchezaji kutoka Nigeria aliefunga Bao 5 Mwezi Desemba, amewabwaga Mesut Özil, Marko Arnautovic, Riyad Mahrez, Romelu Lukaku na Dele Alli, na kushinda Tuzo ya Mchezaji Bora.
Mechi inayofuata kwa Watford ni ya Ugenini dhidi ya Swansea City.

LIGI KUU ENGLAND

Jumamosi Januari 16
1545 Tottenham v Sunderland              
1800 Bournemouth v Norwich              
1800 Chelsea v Everton              
1800 Man City v Crystal Palace             
1800 Newcastle v West Ham       
1800 Southampton v West Brom           
2030 Aston Villa v Leicester
Jumapili Januari 17
1705 Liverpool v Man United                
1915 Stoke v Arsenal                 
Jumatatu Januari 18
2300 Swansea v Watford  

No comments:

Post a Comment