Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa TMAA, Yisambi Shiwa alisema raia mmoja wa kigeni na Mtanzania, walikamatwa wakiwa na madini hayo bila kuwa na kibali chochote cha usafirishaji kama ambavyo Sheria ya Madini ya mwaka 2010 inavyoelekeza.
“Raia huyu wa kigeni ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi kwani tayari ameshafunguliwa kesi mahakamani, alikuwa anasafiri kwenda mji wa Bangkok Thailand na alikamatwa akiwa na madini ya aina mbalimbali ikiwemo almasi, aquamarine, sapphire, green tourmaline, quartz na rhodolite,” alisema Shiwa.
Shiwa alisema tukio lingine, Mtanzania ambaye alikuwa anasafiri kwenda Ujerumani alikamatwa akiwa na madini na kufikishwa katika vyombo vya dola. Alisema katika kipindi cha kuanzia Julai mwaka jana hadi Januari 13 mwaka huu, kumekuwepo na matukio 14 ya utoroshaji madini.
Alisema madini yenye thamani ya Sh bilioni 3.2 yalikamatwa na wakaguzi wa Wakala kupitia Madawati ya Ukaguzi yaliyopo katika viwanja vya ndege vya Dar es Salaam (JNIA), Kilimanjaro (KIA) na Mwanza ambapo yote yalitaifishwa na Serikali.
No comments:
Post a Comment