Friday, 15 January 2016

BAADA YA KOCHA WA SIMBA KERR KUTIMULIWA SULEIMAN MATOLA AZUNGUMZA HAYA

Image result for Suleiman Matola
 
  kocha msaidizi wa zamani wa Simba, Suleiman Matola, amesema Simba imechelewa kumtimua Kocha Dylan Kerr kwani alianza muda mrefu kuiharibu timu

Hivi karibuni Matola aliamua kuondoka mwenyewe Simba na kujiunga na Geita Gold Sports ya Ligi Daraja la Kwanza kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutoelewana kwake na Kerr ambaye ni raia wa Uingereza.
Image result for Suleiman Matola
Simba mapema wiki hii ilitangaza rasmi kuvunja mkataba na Kerr kwa kilichoelezwa kutoridhishwa na mwenendo wa kikosi hicho katika mechi zake za michuano mbalimbali. 

Matola alisema: “Kerr ni kocha mzuri ila nilishawaambia viongozi mapema kuwa hafai ndani ya timu kutokana na yeye kutaka kufuata kile anachokiamini bila ya kushirikiana na wenzake hata kama anakosea.
 
 Image result for Suleiman Matola
“Simba imechelewa kumtimua kwani ameiweka timu mahali pabaya na kama angeondoka mapema usikute klabu ingekuwa pazuri sasa,” alisema Matola.

No comments:

Post a Comment