Yamkini pesa hizo ni zinatumika kuendesha kiyoyozi na mashine mengine ya kusafisha hewa shirika la habari la China Xinhua limeripoti.
Miji mingi nchini China zimeghubikwa na ukungu mkubwa unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi yanayochochewa na hewa mkaa inayotoka viwandani.
Katika miji mingi nchini humo ni vigumu kuona umbali wa mita 100 kutokana na ukungu mzito uliosababisha serikali kuagiza viwanda vifungwe kwa siku kadhaa juma lililopita.
Hata hivyo hakufwata kanuni zinazosimamaia bei ya vyakula wala hakutoa ilani kwa wateja wake.
Maafisa wa mji huo walimlazimisha kufutilia mbali gharama hiyo wakisema hawezi kuwauzia wateja wake ''hewa safi'' shirika la kitaifa la Xinhua linasema.
''Kwa hakika ni wajibu wa Manispaa kuhakikisha mazingira ni masafi lakini sasa wameshindwa kutekeleza wajibu wao na wanamuadhibu mtu ambaye amejitahidi kuhakikisha wateja wake wanapumua hewa safi ''anasema mteja mmoja kupitia kwa mtandao wa Sina Weibo.
No comments:
Post a Comment