Kocha huyo amekua kwenye shinikizo kubwa ya kumtaka kujiuzulu kufuatia kikosi hicho kuchapwa michezo minne mfululizo kipigo cha mwisho kikiwa kutoka kwa Stoke City Jumamosi walipocharazwa 2-0.
Man United wameshindwa kupata ushindi katika michezo minane ya mashindano yote waliyoshiriki msimu huu. Hii ni mara ya kwanza klabu hiyo kufanya hivyo tangu mwaka 1990.
Klabu hiyo kwa sasa imo nambari sita kwenye jedwali na alama tano nyuma ya klabu iliyo nambari nne ligini.
"Mzozo uliopo sasa ni mazingira ambao nyingi (wanahabari) mmechangia," alisema meneja huyo.
"Wachezaji wamejitolea kupambana. Meneja amejitolea kupigana. Wakufunzi vilevile na bodi pia ina imani na wakufunzi na meneja."
No comments:
Post a Comment