Tuesday, 29 December 2015

BAADA YA MAN UNITED KUTOKA SALE NA CHELSEA HAYA NI MANENO YA LUIS VAN GAAL

Image result for van gaal

Meneja wa Manchester United Louis van Gaal, amesema haoni haja ya kujiuzulu baada ya timu yake kutoka sare ya 0-0 na Chelsea uwanjani Old Trafford.
Akizungumza baada ya mchezo kumalizika Van Gaal alisema "kama wachezaji wanaweza kucheza kwa kiwango kile wakiwa kwenye shinikizo hakuna sababu ya kujizulu".
Kocha huyo amekua kwenye shinikizo kubwa ya kumtaka kujiuzulu kufuatia kikosi hicho kuchapwa michezo minne mfululizo kipigo cha mwisho kikiwa kutoka kwa Stoke City Jumamosi walipocharazwa 2-0.
Man United wameshindwa kupata ushindi katika michezo minane ya mashindano yote waliyoshiriki msimu huu. Hii ni mara ya kwanza klabu hiyo kufanya hivyo tangu mwaka 1990.
Klabu hiyo kwa sasa imo nambari sita kwenye jedwali na alama tano nyuma ya klabu iliyo nambari nne ligini.
Van Gaal, anaamini anaungwa mkono na wachezaji na bodi pia.
"Mzozo uliopo sasa ni mazingira ambao nyingi (wanahabari) mmechangia," alisema meneja huyo.
"Wachezaji wamejitolea kupambana. Meneja amejitolea kupigana. Wakufunzi vilevile na bodi pia ina imani na wakufunzi na meneja."

No comments:

Post a Comment