
Ligi Kuu Uingereza
iliendelea usiku wa March 1 kwa michezo mitano kupigwa katika viwanja
tofauti tofauti, miongoni mwa mchezo uliochezwa usiku wa March 1 ni
mchezo kati ya Norwich City dhidi ya Chelsea katika dimba la Carrow Road.
Chelsea walikuwa
ugenini na kuendeleza harakati zao za kupambana na kuhakikisha wanashika
nafasi za juu, licha ya kuwa matumaini yao ya kutetea taji lao la Ligi
Kuu Uingereza yameshapotea, kwani wana tofauti ya point 18 dhidi ya Leicester City anayeongoza Ligi.

Usiku wa March 1 dimba la Carrow Road Chelsea walifanikiwa kuondoka na point tatu muhimu, baada ya goli la dakika ya kwanza la Robert Kenedy na goli la dakika ya 45 la Diego Costa kudhihirisha ushindi, licha ya jitihada za Norwich City kutaka kusawazisha kwa Nathan Redmond kuifungia goli la kwanza dakika ya 68.

Chelsea ambao walifanikiwa kuibuka na ushindi wa 2-1, wapo nafasi ya 8 katika msimamo wa Ligi Kuu Uingereza kwa kuwa na jumla ya point 39 katika michezo ya 28 waliocheza. Chelsea watashuka dimbani March 5 kucheza dhidi ya Stoke City katika mchezo wao wa 29 wa Ligi Kuu Uingereza.
MATOKEO MENGINE HAYA...........
AFC Bournemouth 2 - 0 Southampton
Aston Villa 1- 3 Everton
FT
Sunderland
Crystal Palace
No comments:
Post a Comment