![]() |
Meneja Schmidt alikataa kuondoka eneo la kiufundi |
Refarii mmoja nchini Ujerumani alishangaza wengi baada yake kuondoka uwanjani na kuacha mechi imesimama kufuatia kisa kilichomhusisha meneja wa timu moja iliyokuwa ikicheza uwanjani.
Mechi hiyo ya Bundesliga dhidi ya Borussia Dortmund ilicheleweshwa kwa dakika nane hivi na ilirejelewa baada ya Schmidt mwishowe kukubali kuondoka eneo la kiufundi.
Schmidt alikuwa amedai kuwa bao la Dortmund, lililofungwa na Pierre-Emerick Aubameyang, halikufaa kukubaliwa.
Mkufunzi huyo wa umri wa miaka 48 alisema mkwaju wa adhabu uliopelekea kufungwa kwa bao hilo haukupigiwa eneo sahihi.
![]() |
Zwayer baadaye alirejea baada ya Schmidt kukubali kuondoka |
Baada ya hilo kushindikana, Zwayer aliondoka uwanjani na kuingia chumba cha kubadilishia mavazi. Alifuatwa na wachezaji.
“Nakubali, nilifanya kosa. Lakini refa angenifafanulia ni kwa sababu gani alikuwa akinifukuza,” Schmidt alijitetea baadaye.
No comments:
Post a Comment