Monday, 7 December 2015

wanne mbaroni kwa picha za mtandaoni

Alisema mizigo hiyo ni mali ya JWTZ na kuagizwa kwake, hakujaanza hivi karibuni kama baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii wanavyoeleza, bali ni matokeo ya hatua zilizochukiliwa na JWTZ kupitia Wizara ya Ulinzi miaka sita iliyopita katika mpango wake wa kujenga uwezo wa JWTZ.
“Tunasikitika kwa tukio hili la watu kujichukulia maamuzi ya kupiga picha kitu ambacho hakikuwahusu na pia kusambaza picha hizo kwenye mitandao ya kijamii na kupelekea kujitokeza kwa maoni ya kupotosha jamii,” aliongeza Mkurugenzi huyo katika JWTZ.
Alisema tabia za kupotosha jamii, zimetokea mara kwa mara na hivyo kuvunja mshikamano uliopo kati ya Serikali na wananchi wake, jambo ambalo jeshi hilo halitalifumbia macho.
Alisema ni kwa msingi huo, wameanza kuwasaka wahusika wote, ambapo tayari watu wanne wapo chini ya ulinzi na watachukuliwa hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine, kutokana na upigaji wa picha hizo na usambazaji wake.

No comments:

Post a Comment