Wednesday, 9 December 2015

VALENCIA YAIFUATA MAN UNITED EUROPA LEAGUE


  Kocha Garry Neville ameanza na ‘mkosi’ baada ya mechi yake ya kwanza akiwa benchi kuishuhudia Valencia ikitandikwa nyumbani kwa mabao 2-0 na Lyon.

Lyon ya Ufaransa ilionekana kibonde kutoka Kundi H, lakini ushindi wake ndiyo umeiokoa Gent isonge mbele 16 bora huku Valencia ikiporomoka kwenda Europa League.


 
Sasa kikosi cha Neville kinakwenda kukutana na timu yake ya zamani ya Manchester United ambayo jana iliporomoka huko.
Neville anaifundisha Valencia akiwa anasaidiwa na mdogo wake, Phil Neville na wote waliowahi kuichezea Manchester United kwa mafanikio makubwa.
H. BABA AIBUKA NA WIMBO WA RHUMBA A+ A- Print Email MWANAMUZIKI wa Kizazi Kipya ‘Bongofleva’, Hamisi Ramadhani ‘H Baba’, ni kama ameamua kubadili staili yake ya muziki kwa sasa kwa kutoka na wimbo mpya wenye mahadhi ya Rhumba. H. Baba anayetambulika kwa staili yake ya cheza kwa ufasaha, sasa ameamua kutoka kivingine kabisa tofauti na mashabiki wake walivyomzoea. Akiongea na Saluti5, H. Baba alisema ni mapema mno kutaja jina la wimbo wake huo mpya anaotarajia kuuachia mwishoni mwa mwezi huu, kwani anataka uwe ‘surprise’ ya mwaka kwa mashabiki wake. “Kuna baadhi ya wasanii wana tabia ya kuiba kazi za wenziwao, hivyo wimbo huu sitautaja jina hadi hapo nitakapokuwa tayari kuuachia,” alisema H. Baba. H. Baba alisema wimbo huo wenye staili hiyo mpya iliyochanganyika na vionjo vya muziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ameurekodia C9 Records iliyo chini ya C9 Kanjenje.

Soma zaidi hapa >>: http://www.saluti5.com/2015/12/h-baba-aibuka-na-wimbo-wa-rhumba.html
Copyright © saluti5
HOMA YA MAFUA YAMTESA MARIAH CAREY A+ A- Print Email MWANAMUZIKI Mariah Carey wa Marekani alilazimika kukimbizwa hospitalini mjini New York, Jumatano iliyopita kutokana na kubanwa na mafua makali. Alilazimika kupatiwa matibabu yanayoambatana na vifaa vya kumtia joto, vitamin pamoja na dawa za kupambana na vidudu vinavyosababisha homa kali na kushindwa kupumua. Kuna uwezekano mkubwa homa hiyo ikampunguzia ratiba yake ya maonesho ambapo Jumamosi iliyopita angetumbuiza New Jersey.

Soma zaidi hapa >>: http://www.saluti5.com/2015/12/homa-ya-mafua-yamtesa-mariah-carey.html
Copyright © saluti5
MWANAMUZIKI Mariah Carey wa Marekani alilazimika kukimbizwa hospitalini mjini New York, Jumatano iliyopita kutokana na kubanwa na mafua makali. Alilazimika kupatiwa matibabu yanayoambatana na vifaa vya kumtia joto, vitamin pamoja na dawa za kupambana na vidudu vinavyosababisha homa kali na kushindwa kupumua. Kuna uwezekano mkubwa homa hiyo ikampunguzia ratiba yake ya maonesho ambapo Jumamosi iliyopita angetumbuiza New Jersey.

Soma zaidi hapa >>: http://www.saluti5.com/2015/12/homa-ya-mafua-yamtesa-mariah-carey.html
Copyright © saluti5

No comments:

Post a Comment