![]() |
| Ni wagombea watano pekee walioidhinishwa kuwania |
Mkuu wa shirikisho la soka la Liberia, Musa Bility, amekata rufaa kwenye mahakama ya kuatatua mizozo ya michezo (Cas) akilalamikia kuzuia kuwa mgombea uchaguzi wa urais Fifa.
“Uamuzi wa Fifa si wa haki, unaudhi na kusikitisha,” Bility alisema kupitia taarifa.
“Nimekata rufaa kwa Cas nikiwahimiza washughulikie rufaa yangu kwa dharura.”
Bw Bility, mwenye umri wa miaka 48, amekosoa uhalali wa vigezo vilivyotumiwa, na pia ameitaka Fifa kufanya wazi matokeo ya uchunguzi kuhusu kila mgombea kwa mashirikisho yote 209 ya soka, badala ya kuyafungia.
Uchaguzi wa kuamua mrithi wa raia anayeondoka Sepp Blatter utafanyika Februari 26.

No comments:
Post a Comment