Siku ya Ijumaa ya June 10 ndio ilikuwa
siku ambayo wapenzi na mashabiki wa mchezo wa ngumi, walipata nafasi ya
mwisho ya kufanya ibada ya pamoja ya katika ukumbi wa Kentucky Freedom kumuombea bondia nguli wa mchezo wa ngumi duniani hayati Muhammad Ali.
Familia ya hayati Muhammad Ali ilikusanyika pamoja na umati wa watu unaotajwa kufikia 14000 na kufanya ibada ya pamoja ya saa moja, kwa ajili ya kumuombea Muhammad Ali, ibada ambayo ilihudhuriwa na wake zake pia Khalilah Camacho-Ali na Veronica Porche-Ali.
Bondia wa zamani Lennox Lewis
Bondia Sugar Ray alikuwepo pia
Mke wa tatu wa Muhammad Ali ‘Veronica Porche’
Mke wa pili wa Muhammad Ali ‘Khalilah Camacho’
No comments:
Post a Comment