Tuesday, 29 December 2015

WANAKIJIJI WA KIJIJI CHA LUKANI KILICHOPO WILAYA YA KILOLO WAMKATAA AFISA MTENDAJI KUTOKANA NA UTENDAJI MBOVU

Image result for WANANCHI WA VIJIJI

Wananchi wa kijiji cha Lukani katika Kata ya Ngu’ruhe wilaya ya kilolo mkoa wa Iringa wamemkataa mtendaji wa kijiji hicho katika mkutano wa kijiji uliofanyika kijijini hapo kutokana na utendaji mbovu wa kiongozi huyo.


Tukio hilo limetokea  katika mkutano wa hadhara ulioudhuriwa pia na mbunge wa jimbo la Kilolo VENANCE MWAMOTO,diwani wa kata hiyo, mwenyekiti na viongozi mbalimbali pamoja na wanakijiji. 

Wananchi wa kijiji cha Lukani wamesema mtendaji huyo ameshindwa kusimamia wananchi kupata pembejeo za kilimo pamoja masuala mbalimbali ya maendeleo ya kijiji hicho.
Kwa upande wake Mtendaji anayelalamikiwa NIKODEMASI KADINDE amesema yeye anafanya kazi kwa ufanisi lakini kuna baadhi ya wajumbe wa serikali ya kijiji wanapandikiza chuki dhidi yake kwa wananchi wa kijiji hicho 

Naye diwani wa kata ya Ngu;ruhe PANCRASI KIHANGA amewataka wananchi kumvumilia mtendaji wa kijiji hicho ili aweze kukabidhi nyaraka za serikali na baada ya hapo watamuhamisha kikazi.

No comments:

Post a Comment