Rais huyo alisusia ufunguzi wa mazungumzo ya amani nchini Uganda siku ya Jumatatu.
Nkurunzinza aliyeshinda muhula wa tatu katika uchaguzi mkuu uliokumbwa na utata na maasi mwezi julai mwaka huu anakana kuwepo kwa visa vya mauaji nchini mwake.
Archbishop wa Gulu, John Baptist Odama, ameiambia BBC kuwa wameiomba serikali ya Burundi kupatia mazungumzo ya amani fursa ya kuwapatanisha mahasimu nchini humo.
John Baptist Odama alisema ''Tunaisihi serikali ichukue hatua za kukomesha mauaji ya kiholela nchini humo.
Tafadhali tunawataka wakomesha mauaji zaidi ya watu.
Njia bora ya kusuluhisha mtafaruku huu ni kwa serikali na upinzani kujadiliana.
Mazungumzo ya amani labda ndio suluhisho la kudumu la pekee la mzozo huu.'' alisema Odama.
Umoja wa Mataifa unakadiria watu 400 wameuawa tangu machafuko kuzuka mwezi Aprili Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kwamba angewania urais kwa muhula wa tatu.
Baadhi ya mambo ambayo muungano huo unaruhusiwa kuingilia kati kuzuia ni uhalifu wa kivita, mauaji ya halaiki na uhalifu dhidi ya binadamu.
Maafisa wa UN wameonya kuwa nchi hiyo inakabiliwa na hatari ya kutumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Jeshi lilisema watu 87 waliuawa.
AU hata hivyo bado itahitaji kupewa idhini na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kati.
chanzo bbc
No comments:
Post a Comment