Monday, 28 December 2015

MABARAZA YA BIASHARA NI SULUHISHO KWA CHANGAMOTO ZA KIBIASHARA



Image result for SIGN OF TCCIA 

Wakulima,wafanyabiashara  na wamiliki wa viwanda mkoani Iringa wameshauriwa kutoa ushilikiano pale wanapohitajika kwaajiri ya kujadili kero zinazowakabiri.

Hayo yamesemwa na afisa mtendaji wa TCCIA mkoa wa Iringa BW. Jemes Sizia wakati akizungumza na radio country fm ofisini kwake na kuongeza kuwa malengo waliyonayo kwa sasa ni kuanzisha mabaraza ya biashara katika mkoa na wilaya ili kuweza kusaidia kutatua kero mbalimbali kwa wafanyabiashara, wakulima na wamiliki wa viwanda.

Aidha Jemes amesema mabaraza yatakayo anzishwa yatasaidia kuwa na mazingira rafiki kwa wafanyabiashara ambapo itasaidia kuboresha biashara zao na kuboresha ulipaji wa kodi kwa serikali.

Pia Jemes amesema serikali nayo inanafasi kubwa ya kushilikiana na tahasisi mbalimbali nchini kwa kuondoa vikwazo na kutengeneza mazingira mazuri kwa wafanyabiashara ili waweze kunufaika na kazi zao na kuondoa suala la kuyonywa kwa wafanyabiashara.

Hata hizo TCCIA  wanampango wa kuendeleza kampeni ya matumizi sahihi ya mizani na vipimo kwa wakulima na wafanya biashara  hasa kwa nchi nzima

No comments:

Post a Comment