“Bado
tunasubiri Genk wamalizane na Mazembe, huwezi kumsainisha mchezaji wa
timu nyingine mkataba. Lakini mimi nimeshamalizana na Genk kwa maana ya
makuabaliano, suala la mkataba litafuatia,” alisema Samatta.
Samatta
anatarajia kuondoka nchini kwenda Nigeria katika tuzo za mchezaji bora
wa Afrika yeye akiwa anawania tuzo ya wachezaji wanaocheza ndani ya bara
la Afrika.
Samatta
anapewa nafasi ya kutwaa tuzo hiyo kutokana na kuisaidia TP Mazembe
kutwaa ubingwa wa Afrika pamoja na yeye kuibuka mfungaji bora.
Tamasha
maalum la tuzo hizo limepangwa kufanyika Januari 7 jijini Lagos,
Nigeria ikiwa ni siku mbili tu baada ya Samatta kutua nchini humo.
No comments:
Post a Comment