Wednesday, 30 December 2015

BENTEKE AIFIKISHA LIVERPOOL KWA MAN UNITED

 
 Image result for BENTEKE


BAO pekee la Christian Benteke limewapa Liverpool ushindi wa Bao 1-0 walipocheza huko Stadium of Light na Sunderland katika Mechi ya mwisho kabisa ya Ligi Kuu England.
Bao hilo lilipatikana Dakika 1 tu baada ya Kipindi cha Pili kuanza kwa Nathanial Clyne kupenyeza Mpira mbele na Adam Lallana kuugusa tu na kumkuta Christian Benteke aliefunga na kuipa Bao Liverpool.
Ushindi huu umewaweka Liverpool Nafasi ya 7 wakiwa Pointi sawa na Man United waliowazidi kwa ubora wa magoli.

No comments:

Post a Comment