MECHI
ya BPL, Ligi Kuu England, kati ya Manchester United na Bournemouth
iliyokuwa ichezwe Uwanjani Old Trafford imefutwa kwa sababu za
kiusalama.
Mechi ni ya mwisho ya Ligi kwa Timu hizo mbili na imefutwa baada ya
kugundulika kwa mzigo wa mashaka kwenye Jukwaa la Stetford End na
kuwafanya Walinzi kuwatoa nje ya Uwanja Mashabiki waliokuwa Jukwaani
hapo pamoja na wale wa Jukwaa la Sir Alex Ferguson huku Polisi na Mbwa
spesho wa Polisi wakipita kila sehemu kuchunguza.
Baada ya muda mfupi Washabiki wakatangaziwa kuwa Mechi hiyo imefutwa na haijajulikana lini itachezwa.
Man United walikuwa wanahitaji kushinda Mechi hii na Man Cuty
kufungwa hii leo ili waipiku Man City katika Nafasi ya 4 ili wacheze
UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Hadi Mapumziko City wakicheza Ugenini huko Liberty Stadium walikuwa Sare 1-1 na Swansea City.
LIGI KUU ENGLAND
No comments:
Post a Comment