Wednesday, 2 March 2016

CHELSEA YAPATA USHINDI WA 3 MFULULIZO, BWANA MGOGO AWEKA RECORD EPL

Kenedy


Chelsea wameshinda mechi yao ya tatu mfulizo kwenye Premier League na mashabiki wa timu hiyo tayari wameanza kuwa na matumaini huenda timu yao ikamaliza msimu wa ligi ikiwa kwenye top six.
Magoli ya Kenedy na Diego Costa yaliisaidia Chelsea kuibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Norwich bao la Norwich likifungwa dakika za lala salama na Nathan Redmond.
Chelsea sasa wamepanda hadi nafasi ya nane kwenye msimamo wa Premier League juu ya Liverpoo ambayo kwa sasa bado inapambana kupata matokeo mazuri huku kikosi hicho kinachonolewa na mjerumani Jurgen Klopp kikiwa na mechi mbili mkononi.
Story kubwa kwenye mchezo huo ni kuhusu Kenedy mchezaji wa Chelsea ambaye alifunga goli lake la kwanza kwenye Premier League. Pia ndiyo goli la mapema zadi kufungwa hadi sasa kwenye msimu huu, likiwa limefungwa sekunde ya 39 tu tangu mchezo kuanza.

No comments:

Post a Comment