Licha ya hakikisho kutoka kwa maafisa wa usalama, ni wanafunzi wachache pekee waliorejea chuoni, wengi wao wakiwa wa kujilipia.
Takriban wanafunzi 800 wa kufadhiliwa na serikali, waliokuwa wakisomea katika chuo hicho kabla ya shambulio kutokea, walihamishiwa chuo kikuu cha Moi mjini Eldoret.

Kituo cha polisi kimejengwa ndani ya chuo kudumisha ulinzi.
Maafisa zaidi ya 20 wa polisi watakuwa wakikaa humo.
No comments:
Post a Comment