Tuesday, 8 December 2015

WENGER AZUNGUMZA MANENO HAYA KUELEKEA MCHEZO WA UEFA SOMA HAPA

Image result for WENGER         

UEFA CHAMPIONZ LIGI

Mechi za Mwisho za Makundi
RATIBA
**Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku, isipokuwa inapotajwa
Jumatano Desemba 9
KUNDI E
Bayer Leverkusen v Barcelona     Roma v BATE Borislov                
KUNDI F
Dinamo Zagreb v Bayern Munich           
Olympiakos v Arsenal                 
KUNDI G
Chelsea v FC Porto           
Dynamo Kiev v Maccabi Tel Aviv           
KUNDI H
KAA Gent v Zenit Saint Petersburg                  
Valencia v Lyon               

ARSENE WENGER amesisitiza Arsenal wanaingia Jumatano Uwanjani Karaiskaki huko Piraeus, Ugiriki kuwavaa Olympiakos katika Mechi ya mwisho ya Kundi F la UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL ambayo lazima washinde ili wafuzu Raundi ya Mtoano ya Timu 16, wakiwa hawaogopi kitu.
Lakini si ushindi tu bali wanapaswa kuipiku Rekodi ya Olympiakos waliyoiweka Emirates ambako waliichapa Arsenal 3-2 katika Mechi ya kwanza.
Hivyo, ikiwa Arsenal watashinda kwa Bao 1-0 au 2-1 watatupwa nje.
Ikiwa Arsenal hawatafuzu basi watatupwa nje na kulazimika kucheza UEFA EUROPA LIGI kwa vile watakuwa Nafasi ya 3.

KUNDI: F:
Olympiacos (Pointi 9) v Arsenal (6)
Dinamo Zagreb (3) v Bayern München (12, Imeshafuzu)
-Bayern ndio Mabingwa wa kundi.
-Olympiacos waliifunga Arsenal 3-2 huko Emirates na hivyo Arsenal wanatakiwa wapate ushindi bora zaidi ya huo dhidi ya Olympiakos watakapokutana huko Athens.
-Dinamo wako nje.

Arsenal wamefuzu kucheza Raundi ya Mtoano ya UCL kwa Miaka 15 mfululizo hadi sasa lakini hali ngumu ya sasa kwenye Kundi lao halikumfadhaisha Meneja wao Arsene Wenger ambae amejipa moyo.
Wenger amesema: “Tutafanya kila jitihada tufuzu. Ukitaka kuruka kihunzi hufikirii nini kitatokea ukikosea!”

No comments:

Post a Comment