![]() |
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi MkuuDkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la Kikosi cha Jeshi la Wanamaji. |
Rais Kikwete amesema kuwa Mzee Mandela alikuwa mtu wa kipekee kutokana na ujasiri wa kutetea haki za wanyonge licha ya kupata mateso kutoka kwa makaburu.
Hayati Mandela atakumbukwa kwa moyo wa kusamehe na kupinga ubaguzi wa Rangi akiwa katika harakati za ukombozi na hatimaye Afrika Kusini ikawa huru.
Maadhimisho hayo yamefanyika katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam ambapo Rais Kikwete alikagua gwaride maalumu la vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama.
Tanzania Bara ilipata uhuru wake mwaka tarehe 9 Desemba 1961 kutoka kwa wakoloni wa Uingereza na Baba wa Taifa hilo Hayati Julius Kambarage Nyerere anakumbukwa kwa harakati zake za kuhakikisha Taifa hilo linakuwa huru.
Kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika kwa mwaka huu inafanyika chini ya kauli mbiu isemayo “Vijana ni Nguzo ya Rasilimali Watu, Tuwaamini, Tuwawezeshe na Tuwatumie kwa Manufaa ya Taifa Letu.
No comments:
Post a Comment